UMOJA WA SHIDA NA RAHA
Uhusiano kati ya Wachagawote na USHIRA
Jukwaa la Wachagawote linatambulisha na kutangaza USHIRA kama sehemu ya jumuiya pana ya vikundi vya Wachaga. Wachagawote haihusiki na uendeshaji wa ndani, michango, maamuzi ya kifedha au uongozi wa USHIRA. Kutangazwa kwa USHIRA ndani ya Wachagawote ni kwa madhumuni ya taarifa kwa jamii, si usimamizi au umiliki. Mawasiliano yote yanayohusu uanachama, michango, vikao na fao la pole au pongezi yaelekezwe moja kwa moja USHIRA kupitia taratibu zake rasmi.
Utangulizi
Umoja wa Hiari
USHIRA ni umoja wa hiari wa kijamii, usio wa kisiasa wala kidini, wenye lengo la kujenga mshikamano katika shida na raha.
Makao Makuu
Dar es Salaam, Tanzania. Hushughulikia wanachama kutoka maeneo mbalimbali ya U-Chagga wanaoishi Dar es Salaam na kuendelea.
Lugha Rasmi
Kiswahili ndiyo lugha rasmi ya mawasiliano na nyaraka zote za Umoja.
Shida Tushirikiane, Raha Tugawane
Daima Tupo Pamoja
Malengo ya USHIRA
Malengo mahsusi ya umoja kama yalivyoainishwa katika Katiba
Kusaidiana kifedha na kihisia pindi msiba au tatizo linapotokea
Kushirikiana katika matukio ya furaha kwa kupongeza kwa utaratibu rasmi
Kukuza mshikamano kupitia mikutano, mawasiliano ya kidijitali na ziara
Kuendeleza elimu ya fedha na shughuli ndogo za kijamii/kiuchumi kwa maamuzi ya kikao
Uanachama
Sifa za Kujiunga
- Awe mtu mzima (18+), mwenye akili timamu
- Hakuna ubaguzi wa dini, jinsia, elimu au kazi
- Lazima awe na Asili ya Kichaga
- Akubali Katiba na kanuni za Umoja
Haki za Mwanachama
- Kuhudhuria na kupiga kura katika mikutano
- Kuchagua na kuchaguliwa uongozi
- Kupata fao la pole/pongezi akiwa "mwanachama hai"
- Kupata taarifa rasmi za Umoja (ikiwemo taarifa za kifedha)
Wajibu wa Mwanachama
- Kuheshimu Katiba na maamuzi halali
- Kulipa michango ya tukio kwa wakati
- Kuilinda heshima ya Umoja
- Kumkaribisha mwanachama mpya
Kusitishwa au Kuondolewa Uanachama
Michango ya Tukio
Kila mwanachama hai huchangia kwa mujibu wa Katiba
POLE
Msiba/Ugonjwa
PONGEZI
Furaha
Ulinzi na Ustahiki
Mwanachama asiye hai wakati wa tangazo halazimiki kulipa na hapokei mafao hadi arudishe hadhi yake kwa kulipa yaliyostahili + faini.
Uongozi na Kamati
Muundo wa uongozi kwa mujibu wa Katiba (Mia 3)
Viongozi Wakuu (Sekretarieti)
Mwenyekiti
Aongoze vikao, awasilishe msimamo wa Umoja
Katibu
Kumbukumbu, wito wa vikao, mawasiliano
Mweka Hazina
Mapato/matumizi, vitabu vya hesabu
Muda wa Uongozi
Mia 3 • Uchaguzi kila baada ya miaka 3
Kamati za Kudumu
Fedha na Ukaguzi
Ukaguzi wa ndani, kuhakikisha uwazi wa fedha
Jamii
Masuala ya pole/pongezi na ustawi wa wanachama
Maadili na Nidhamu
Kushughulikia ukiukaji wa maadili
TEHAMA na Mawasiliano
Kusimamia mikondo rasmi na faragha ya taarifa
Mikutano na Akidi
Aina za Mikutano
- Mkutano Mkuu wa Mwaka (AGM) - Mara 1 kwa mwaka
- Mkutano Mkuu wa Uchaguzi - Kila miaka 3
- Mkutano Maalum/Dharura - Inapobidi
- Vikao vya Kawaida
Notisi za Mikutano
- AGM: Siku 14 kabla
- Mkutano wa kawaida: Siku 7 kabla
- Dharura: Siku 2 (au muda utakaoruhusu)
- WhatsApp, SMS, Barua pepe, au ukurasa rasmi
Akidi (Quorum)
1/3 ya wanachama hai
1/2 ya wanachama hai
Fedha na Ukaguzi
Vyanzo vya Mapato
- Kiingilio (TSh 50,000)
- Michango ya tukio (Pole/Pongezi)
- Harambee na ruzuku halali
- Mapato ya shughuli ndogo zilizoidhinishwa
Hakuna ada ya mwezi
Akaunti ya Benki
Fedha zote za Umoja ziwekwe benki
Saini mbili kati ya tatu:
Mwenyekiti
Katibu
Mweka Hazina
Matumizi > TSh 1,000,000: Idhini ya Sekretarieti
Matumizi > TSh 5,000,000: Idhini ya Mkutano
Mwaka wa Fedha
Julai hadi Juni - Taarifa za kifedha huwasilishwa katika kila Mkutano Mkuu
Maadili na Nidhamu
Uadilifu
Kutenda kwa uaminifu na kusimamia haki
Uwazi
Taarifa wazi kwa wanachama wote
Kuheshimiana
Heshima kati ya wanachama na viongozi
Ukiukaji wa maadili hushughulikiwa na Kamati ya Maadili na Nidhamu, haki ya kusikilizwa ikidumishwa. Kuondolewa kunahitaji kura ya 2/3 ya wanachama waliopo kikaoni baada ya kujitetea.
TEHAMA na Mawasiliano
WhatsApp Group
Mikondo rasmi ya wanachama
Facebook Page
Taarifa rasmi za Umoja
Mikutano Kidijitali
E-Voting inaruhusiwa kwa maamuzi yote
Wachagawote na USHIRA
Wachagawote
Jukwaa huru la kidijitali
- Linatangaza taarifa
- Linatambulisha vikundi
- Halihusiki na uendeshaji
USHIRA
Umoja wa Shida na Raha
- Unaongozwa kwa Katiba
- Uongozi wake unajitegemea
- Maamuzi ya ndani ni yake
Kutangazwa kwa USHIRA ndani ya Wachagawote ni kwa madhumuni ya taarifa kwa jamii, si usimamizi au umiliki.
Jiunge na USHIRA Leo!
Kuwa sehemu ya umoja unaothamini mshikamano katika shida na furaha. Kwa pamoja tunajenga jamii yenye nguvu.